Tuesday, September 28, 2010

UCHAGUZI NA MIMI PART3: CCM INACHEZEA MAISHA YA MTANZANIA

Leo niliamua kupitia kwenye website ya chama tawala kutaka kujua sera yao kuu kwenye uchaguzi mkuu. Nilitaka kufahamu kama kuna mpango wowote wanaotegemea kuufanyia kazi kusaidia kuondokana na umasikini. Nilichokutana nacho huko kilikuwa ni kituko.

Naelewa ya kwamba nimeelemea upande mmoja kwenye swala zima la siasa ya Tanzania lakini si bila kuwa na sababu. Nitaorodhesha vichwa vya habari kutoka kwenye website ya CCM na mtu yeyote anayefikiri ninakosea kuviita vituko karibu unikosoe. Tuanzie na hiki kichwa cha habari "Tutawakopesha wavuvi zana za kuvulia " halafu nitanukuu maneno haya chini yake"RAIS Jakaya Mrisho Kikwete na Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu amesema kuwa endapo atachaguliwa tena ataanzisha mpango maalum wa kuwakopesha zana wavuvi katika maziwa ya Tanzania".


"Aidha, Rais Kikwete amewatangazia majambazi wanaofanya uharifu, kushambulia na hata kuua wavuvi katika maziwa ya Tanzania kuwa sasa kiama chao kimefika".Kweli? Umekaa madarakani miaka mitano leo hii ndio unawakumbuka hawa wavuvi? Utawarudisha wale waliouwa na majambazi? Hii ni aibu, Kusimama mbele ya watu na kuwadanganya kwamba utawasaidia wakikuchagua tena wakati muda wote huu hukuwajali.
Badala ya kuwachosha na maandishi yalioyobakia nitaviorozesha vichwa vya habari vilivyobaki ili niweze kurudi kwenye point muhimu.
"Mkutano wa Kampeni Makete: JK akaa vumbini na mlemavu wa viungo "
"Mkutano wa Kampeni Loliondo: JK aahidi kupunguza tatizo la maji Wilayani Ngorongoro"
"Mkutano wa Kampeni Ifunda – JK Awasihi Watanzania Kuepuka Siasa za Ubaguzi "

Nimeviacha vichwa vya habari vingine kwa sababu havisemi chchote cha maana ki msingi wa kuelezea ni nini sera ya CCM kwenye uchaguzi mkuu. Kwenye kila kampeni inayofanywa na Kikwete kinajadiliwa kitu tofauti kutokana na wapi alipo. Hili ni jambo zuri kwa sababu kila kaya inatatizo lake kutokana na wanachojishuhulisha nacho. Lakini tatizo la mataizo makuu ya watanzania hayajadiliwi.
Watanzania wote wanashea UMASIKINI. Ndio kunawale wanasema hapana kunamatajiri bongo lakini waulize kama wanafurahia maisha yao? Huwezi kusema wewe ni tajiri na unamaisha mazuri lakini umeme unakatika kila leo sawa na msela wa uswazi,tofauti pekee unatumia jenereta. Huwezi kusema kunamatajiri wakati hawalali kwa amani kwa kuhofia majambazi. Huwezi kusema kuna matajiri wakati maji ya bomba hakuna wanategemea maji ya tank. Huwezi kusema kunamatajiri wakati wote tunabanana kwenye miundo mbinu mibovu.
Baada ya miaka yote hii ya kuwa chama tawala, miaka yote hii ya kutawala bunge. Ni kweli unaomba uchaguliwe tena uwape wakazi wa loliondo maji? wakazi wa Dar kwa ujumla na mikoa yote iliyobaki utawapa maji lini? Eti JK akaa mavumbini na mlemavu umuhimu wa hilo tukio ni nini? JK anasera gani za kuwalinda walemavu? hicho ndio kitu ningependa kujua na sio kukaa chini na mlemavu halafu unamuacha chini.
Bado sijapitia vyama vingine kuona sera zao ila I hope haziko rejareja namna hii. Watanzania inabidi tuache ushabiki wa kwenda kumshangilia mtu ambaye hana nia ya kuinyanyua nchi badala yake anakuja na wachekeshaji na wasanii wa kizazi kipya kukwepa maswala ya kweli yanayomkabili mwananchi. Ni muhimu kuamua kuchagua maendeleo badala nani alitudondoshea pati nzuri zaidi.

Sunday, September 19, 2010

Nafikiri nihame timu sasa

Sir Alex Ferguson was indebted to the "genius" of Dimitar Berbatov after the Bulgarian's brilliant hat-trick floored Liverpool at Old Trafford.
Every single member of the United side had need to thank Berbatov at the end after they had tossed away a two-goal advantage against Merseyside opposition for the second weekend running, only for the former Tottenham man to net the winner six minutes from time.

In some very perceptive programme notes, Ferguson suggested to lose a winning position once was bad luck, twice is downright careless.

Now Liverpool can be added to Fulham and Everton as teams United have thrown winning positions away against this season.

They were only spared the sight of Ferguson's fury because of Berbatov, whose header denied Liverpool, who had levelled through Steven Gerrard's double.

The other part of Ferguson's pre-match missive was the declaration that "you must have faith and we are being rewarded this season for our confidence in a player who has a touch of genius about him".

Genius was an apt word to describe Berbatov's contribution, in particular the astonishing overhead kick that had put United two ahead midway through the second-half of a slow burner of a game that eventually turned into a classic.

Ferguson is not the only one in these parts who still feel this is the biggest fixture of the Premier League calendar.

Chelsea, Arsenal and even Blackburn may have won the title since Liverpool last did so in 1990. But with their 18 league championships and five European Cups, they remain the most successful English side, even if United have now joined them on the domestic front.

The atmosphere was crackling at kick-off, although the early action failed to match it.

United did create one excellent opportunity, which Nani wasted when he fired wide after Wayne Rooney's shot had bounced kindly for him after striking Gerrard.

But the game was low on incident until Berbatov broke the deadlock by nodding home Ryan Giggs' corner at the near-post.

TV replays did not show Fernando Torres in a good light.

His performance at Birmingham last week was branded "diabolical" by TV pundit and former Liverpool skipper Jamie Redknapp.

Clearly needing a goal, Torres was again struggling to make an impact.

New United captain Nemanja Vidic, who has suffered more than most at the feet of a man who remains one of the world's best strikers, tidied up one opportunity that had come Torres' way via a fortunate bounce off World Cup final referee Howard Webb.

The Liverpool forward also trundled a disappointing shot way off target after managing to get a quarter of a yard in front of Vidic as the pair turned on the edge of the area.

All this was forgivable. Allowing Berbatov, who had already got in front of the former Atletico Madrid star as Giggs strode up to take the corner, just to stoop for it unchallenged, would not have impressed Roy Hodgson very much.

If defensive questions needed to be asked about that, there was nothing more to do than simply admire Berbatov's brilliance when he doubled his side's lead just before the hour.

It was almost impossible to believe it took just two touches to get Nani's right-wing cross into the net.

But it was precisely that. The first to control with his knee. The second to dispatch an overhead kick which left Pepe Reina rooted to the spot as it bounced in off the crossbar.

In any normal season, the contest would have been over.

However, there is a fallibility about United just now that clearly refuses to rectify itself no matter how harsh Ferguson's words.

The rashness with which Jonny Evans lunged in on Torres as the striker checked back inside the box gave lie to the theory United can operate effectively without Rio Ferdinand, overlooked for the captaincy and missing with a virus.

On the second occasion, John O'Shea could count himself mightily relieved Webb did not reach for the red card once he decided the Irishman had dragged Torres to the ground just outside the box.

The consequences of Webb's ruling would be felt in the eventual outcome.

With both situations though, Gerrard found the corner of United's goal with precision, racing gleefully to the ecstatic visiting fans the second time around to hail a position he could not have expected his team would be in 10 minutes previously.

It looked like United had blown it. Berbatov had other ideas and rose to meet O'Shea cross to give his side victory.

Sunday, September 19, 2010
Manchester United 3
Liverpool 2 FT
Wigan Athletic 0
Manchester City 2 FT
Chelsea 4
Blackpool 0 FT

Wednesday, September 15, 2010

Uchaguzi na mimi. part 2

Mara ya mwisho kuandika kuhusu uchaguzi ilikuwa kabla Sugu hajachukua fomu za ubunge lakini alikuwa ameshatangaza nia yake ya kuua[ Ruge upo hapo] Slaa alikuwa hajajua kama ndio atakuwa mgombea wa uraisi wa Chadema lakini alikuwa ameshaoa mke wa mtu na kama kawa CCM walikuwa wanaendelea kufanya serkali na chama kuwa ni kitu kimoja.

Mimi sio mwandishi wa magazeti kwa hiyo ninaelemea upande mmoja na wala hilo sikatai. Mimi ninaweza kusema kuwa na bahati ya kuwa mmoja wa watu wenye upeo tofauti kuhusu hali nzima ya siasa na maisha ya mtanzania na nina bahati pia ya kuwa na marafiki walio kwenye level hiyo hiyo kwa hiyo sihitaji sana kulazimisha point kwa sababu wasomaji wangu wananielewa. CCM imekuwa madarakani kwa muda mrefu sana kushindwa kuleta maendeleo. Kwa katiba ya Tanzania tunategemea chama tawala kifanye mabadiliko ya kimaendeleo kwa miaka mitano kikishindwa mwingine apewe nafasi. CCM imeshindwa sasa kwa nini hatuwapi wengine nafasi?

Niliandika kwenye post ya kwanza sababu zinazofanya CCM inakuwa gumu kutoka madarakani. Kwa wale ambao hamkupata kusoma hiyo post basi kwa kifupi pamoja na mambo mengine mengi ni kwamba baada ya mfumo wa chama kimoja kufa CCM iliendelea kushikilia vitega uchumi vyote walivyokuwa navyo ambavyo vinatakiwa kuwa mali ya wananchi. Chama na serikali vilikuwa ni kitu kimoja,wananchi walijenga viwanja,kumbi za mikutano na kadhalika kwa sababu walikuwa hawana hiari. Kwa msingi huo baada mfumo huo kufa serikali ilitakiwa irithi hivi vitega uchumi badala yake wakakiachia chama. Hii imesababisha mizani kuelemea upande mmoja kwa sababu vyama vingine vyote vimeanzia kwenye sifuri huku CCM wakianzia kwenye tisini na tisa.

Leo hii nata niwapongeze CHADEMA kwa sababu wameonyesha nia yao ya dhati ya kumthamini mtanzania na sio tu tamaa ya madaraka. Kwenye chaguzi zilizopita ilikuwa ni kawaida kwa mwenyekiti wa chama kuwa ndio mgombea wa uraisi lakini CHADEMA wamelibadilisha hilo kwa kumweka mtu anayekubalika na wanachi wengi wenye akili timamu. Vile vile vijana wengi wamejitokeza zaidi kwenye medani ya siasa [kila la heri Mr 11] hii inaonyesha imani iliyopo kwenye chama hiki. CCM ina vijana wao[ the next generation ya mafisadi] wanaonadiwa kwa nguvu sana na this generation, kwa hiyo mchuano utakuwa ni mkali.

Kwa kumalizia napenda niwakumbushe wote umuhimu wa kupiga kura. Siku ya uchaguzi mkuu usikubali mwenzio akuamulie nani akutawale bali amua wewe mwenyewe. kura moja inaweza badilisha nchi.

Umaarufu wa Chadema waongezeka

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimepata umaarufu mkubwa na kuandikwa zaidi na vyombo vya habari hapa nchini, baada ya kumteua Dk. Willibrod Slaa, kuwa mgombea wake wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka huu.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) nacho kimepewa nafasi kubwa ya kuandikwa katika kipindi hiki cha kampeni zilizoanza Agosti 20 mwaka huu kuliko vyama vingine hapa nchini.

Hayo yamebainika katika utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti ya Kimataifa ya Synovate na matokeo yake kutolewa kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam jana.

Kwa mujibu wa taasisi hiyo, kabla ya kutangazwa mgombea huyo, Chadema kilikuwa kikiandikwa katika magazeti, kutangazwa kwenye redio na kuonyeshwa katika runinga mbalimbali hapa nchini kwa kiwango kidogo .

Akizungumza na waandishi wa habari jana kuhusiana na utafiti huo, Meneja wa Huduma za Wateja wa Synovate, Jane Meela, alisema katika utafiti wao wamebaini kuwa baadhi ya vyombo vimeandika habari zao kwa haki, vingine kwa kupendelea chama kimoja na vilivyobaki havikuwa upande wowote. Alisema vyombo vingi vya habari vya serikali, chama na vile vya binafsi vilikiandika zaidi CCM kuliko vyama vingine vya siasa .

Aliongeza kuwa taasisi yake ilifanya utafiti kwa kuangalia vituo 10 vya runinga, magazeti 36 na vituo vya redio 31 katika mikoa tofauti nchini.

Aidha, utafiti huo umebaini kuwa suala la amani lilijadiliwa na watu mbalimbali kwa asilimia 28, rushwa 21, uchumi 15, elimu 12, kilimo saba, afya sita, watu wasiojiweza sita, haki za binadamu tatu na utalii na ajira vilishika nafasi sawa kwa kupata asilimia moja.

Taasisi hiyo pia hufanya utafiti wa masuala mbalimbali yanayohusu jamii na kutoa matokeo yake kwa vyombo vya habari.

CHANZO: NIPASHE